MCHUMBA WANGU NILIMPATA KANISANI…. LAKINI MACHO YANGU
YALINIDANGANYA!!!>>>>
Pasaka hii ilikua mbaya sana kwangu maana sikuwa na furaha
ila machungu mara mbili. Kwanza kwa kufiwa na msanii wetu lakini kikubwa zaidi
huu ndio wakati nilipothibitishiwa kuwa mpenzi wangu ambaye nilitarajia kumuoa…Anasaliti
penzi langu..
Ilikua Jumamosi ya pasaka ambapo nilipata ugeni
nyumbani.mgeni mwenyewe ni huyu mchumba wangu ambaye katka wiki iliyotangulia
nilipata hisia kuwa ananisaliti hivyo tukahitilafiana nikaamua kuwa mbali naye
kwa muda ili kutafuta ukweli kwa vyanzo vingine maana sasa naamini kuwa
lisemwalo lipo…kama halipo laja.
Siku hii alipokuja alikuwa na lengo la kujaribu kunilainisha
nibadili msimamo wangu na kuondoa mawazo nilokuwa nayo juu yake….mambo yakawa tofauti
sana wala sikutarajia kusikia yale nilosikia!!!!!
Nilijiuliza mambo mengi sana …Ni huyu ambaye nilimuona kwa
mara ya kwanza kanisani nikampenda???????...Ni huyu ambaye ni mkimya muda wote
ambaye hata sura yake ni ya upoleee??????
Iliniuma sana sana sana sana hata siwezi kuelezea baada ya
kusikia hayo nilosikia…..Mmmh! We acha tuu inaumaaaaa!
Kwa sasa nimemwacha aendelee na hao watu wate ila kwa kweli
inaniuma mno na wala siwezi kueleze….Lazima niseme kweli ninaumia mnoooo siwezi
kusema…
Najua Bado Nampenda sana kutoka ndani lakini Moyo Wangu
unakataa kabisa kuamini kuwa naweza kumuoa mwanake wa namna hii……
Tafadhali nishauri nifanyeje!!????
Wadau mchango wenu unahitajika katika hili....
ReplyDeleteDah...Aisee nakuonea huruma sana kaka yangu...Lakini ndo ujue sio kila king'aacho ni dhahabu, vingine ni rangi yake tuu. huyo dada kwa vyovyote vile sio mwaminifu hata akifanywaje! Yaani kama ni samaki sio aliyechina bali aliyeoza, maana hata ndimu haiwezi kukata harufu yake mbaya na wala hawi mtamu hata chembe..Mie nakushauri wewe achana nae kabisaa, vinginevyo utajuta sana huko mbele..
ReplyDeleteinaonesha inahuzunisha lakini umeiminya sana story yenyewe. mimi naomba kama ungeitoa yoote kabisa ili tuweze kujua tunakushauri vipi. Wewe tushirikishe yoote kabisa ili tujue la kusema kwa uwazi zaidi.
ReplyDelete